Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2020
UVIMBE KATIKA MAYAI  YA MWANAMKE  (Ovarian Cyst) Habari za mda huu ndugu wapenzi na karibuni katika wasaa  mwingine, Leo  tutajadili kuhusu uvimbe katika mayai ya mwanamke au kwa maneno mengine ovarian cyst, Karibuni kama utakuwa na swali lolote unakaribishwa pia. Uvimbe kwenye mayai ya mwanamke (ovary) hutokana na mkusanyiko wa majimaji yanayozungukwa na kuta nyembamba ndani ya mayai ya mwanamke. Uvimbe huu ambao hupatikana ndani ya mayai ya mwanamke ndio unaojulikana kama ovarian cyst. Uvimbe huu kwa sasa kutokana Na mifumo ya maisha Na ulaji umekuwa ukiwatokea wanawake wa umri wowote ule ingawa kwa kipindi cha nyuma  mara nyingi ulikuwa ukionekana kwa wanawake waliofikia kikomo cha umri wa kupata ujauzito.  Lakini kwanza hebu tufahamu juu ya mayai ya mwanamke. Kwa kawaida mwanamke anakuwa na mayai mawili katika mwili wake.  Yai moja upande wa kulia na yai jingine upande wa kushoto kwake.  Mayai haya hupatikana pembezoni mwa mfuko wa u...

MAGONJWA YANAYOSABABISHA WANAWAKE KUWA WAGUMBA!!*

*MAGONJWA YANAYOSABABISHA WANAWAKE KUWA WAGUMBA!!* P.I.D(pelvic inflammatory disease) na FIBROIDS inavyotesa wanawake na kuwasababishia ugumba. P.I.D NI NINI?? P.I.D ni maambukizi kwenye via vya uzazi wa mwanamke. Ugonjwa huu unaweza kupelekea uharibifu mkubwa kwenye mayai,mfuko wa uzazi,mirija ya uzazi nk  . Pia ugonjwa huu ni moja ya UGUMBA kwa mwanamke.Huu ni ugonjwa unaosababishwa na kutotibu magonjwa ya zinaa kwa ufasaha na kuacha wale bakteria kuendelea kusambaa kwenye via vya uzazi wa mwanamke. *Je utajuaje kwamba huenda umeathirika na ugonjwa huu wa P.I.D ????* *đź’ĄDALILI ZA P.I.D* 👉Maumivu ya tumbo sehemu ya chini au ya juu upande wa kulia 👉Kutokwa kwa uchafu ukeni usio wa kawaida na harufu mbaya(wengi hudhani ni fangas kumbe sio) 👉Maumivu makali na kutokwa na damu wakati wa tendo la ndoa 👉Maumivu wakati wa kukojoa 👉Kutapika na homa 👉Uchovu 👉Kutokwa kwa damu nyingi isiyokuwa na mpangilio wakati wa hedhi au wakati sio wa hedhi( hii dalili kubwa na huw...